|
Karibu Habari mpya Undugu wetu Tunahusiana na nani Jimbo la Biedenkopf Jimbo la Kituntu EKHN KKKT Ujerumani na Tanzania Maeneo ya Kazi Ziara Mbalimbali Jumapili ya Undugu Miradi yetu Mambo ya Umoja Tathmini Wasiliana nasi Wahariri Tovuti nyinginezo Tuunge Mkono
![]() |
EKHN
Wakazi takriban milioni 5 wanaishi katika miji na vijiji vinavyohudumiwa na kanisa hili. Milioni 2 kati yao ni washiriki wa kanisa la EKHN. Aidha watu milioni 1.5 ni wa madhehebu mengine. Kwa mujibu wa Rais wa EKHN, Dr. Peter Steinacker, mambo yafuatayo ni muhimu kwa kanisa: Imani moja na kushiriki katika kutoa huduma za jamii Uhai wa kiroho na ushirikishwaji, kwa njia ya mali na vipawa mbalimbali kote nchini. Kujihusisha na mambo ya kiuchumi na miradi endelevu Kutunza uumbaji wa Mungu, yaani Uwakili. Kupungua kwa waumini wa kanisa la EKHN na makanisa mengine nchini Ujerumani ni changamoto kwa kanisa kuendelea kutoa ushuhuda wake juu ya tumaini katika Yesu Kristo (1. Petro 3:15b). Tangu yalipofanyika mabadiliko katika muundo wa kanisa miaka ya tisini, kanisa lina ngazi kuu tatu ka ifuatavyo: Sharika na mitaa yake Majimbo: Kwa mabadiliko hayo, majimbo yamepewa uwezo zaidi kushughulikia masuala ya ajira na maslahi ya wachungaji, wadiakoni, na watumishi wengine katika nyanja za mahusiano (uekumene) na mambo ya jamii. Kanisa zima (EKHN): Litakuwa na Sinode, yenye vikao vyake mara mbili kwa mwaka, Halmashauri Kuu, Rais wa Kanisa pamoja na Maaskofu 6 wa Mikoa. EKHN na makanisa mengine 23 nchini Ujerumani yanaunda Kanisa la Kiinjili la Ujerumani, liitwalo EKD. EKD ni mwanachama wa Jumuiya ya Makanisa Duniani. EKHN ina mahusiano na makanisa na sharika ngambo ya nchi kama vile: Poland, Jamhuri ya Czech, Italia, Afrika ya Kusini, Tanzania, Ghana, India, Indonesia na Korea ya Kusini Endelea ![]()
|
||